Please Limited time Offer!

Ushairi KCSE Questions And Answers-Questions 6-10

Ushairi KCSE Questions And Answers-Questions 11-15

Ushairi KCSE Questions And Answers-Questions 1-5

USHAIRI WA 6

            Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Wataalamu muwe macho, vuani moto muenge,

      Muenge hicho ambacho, cha watu wenye mawenge,

Mawenge yenye kijicho, kiswahili wakivunge,

Barakala tuwapinge, sichafue kiswahili.

Sichafue kiswahili, barakala tuwapinge,

Apige kila hali, wasiguse tuwainge,

Tuwainge wende mbali, kiswahili tujijenge,

Barakala tuwapinge, sichafue kiswahili.

Sichafue yetu lugha, waharibu Wabanange,

Wabanange iwe nyagha, waiweke tengetenge,

Lugha kuitwa; ulugha, lafidhi watia denge,

Barakala tuwapinge, sichafue kiswahili.

Tuichange heshima, na ulugha tuupinge,

Tuhifadhi kwa salama, na kisingio unyonge,

Kelele za maamuna, si watu ni visinge,

Barakala tuwapinge, sichafue kiswahili.

Kasema sheikh Amri, kiswahili tukisenge,

Kistawi kinawiri, kitumike kwenye bunge,

Hii ni yetu fahari, lugha yetu tuichunge.

Barakala tuwapinge, sichafue kiswahili.

Kikipatwa na maradhi, kwa sindano tukidunge,

Kila jama kutidhi, kipatwe hapo tupunge,

Tukitia mfawadhi, kama kunde na kihenge,

Barakala tuwapinge, sichafue kiswahili.

MASWALI

(a) Ni mtindo gani aliotumia mshairi katika kutunga ubeti wa 1 na 2. (fafanua kwa kutoa mfano)

(alama 4)

(b) Mshairi ametoa mapendekezo kadha katika shairi kuhusu jinsi ya kuimarisha na kuhifadhi lugha ya kiswahili. Taja na ufafanue matano kati ya hayo.                                    (alama 5)

(c) Mshairi anazungumza na akina nani? Anazungumzia nini?                           (alama 4)

(d) Mshairi ametumia tamathali mbalimbali kuwasilisha ujumbe wake. Taja mifano mitatu tofauti ya tamathali hizo.                                                                                                      (alama 3)

(e) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi.         (alama 4)

  • Muenge
  • Barakala
  • Mtawadhi
  • Maamuma.

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA SHAIRI LA 6                                                                                     

8.a)           –      Mtindo wa sabilia: mshororo wa mwisho (kibwagizo) imerudiwarudiwa

–      Pindu: neno moja au sehemu yote ya ubeti wa kwanza hutumiwa kama ukwapi wa ubeti unaofuata                                                                                                                               

  • Anapendekeza wataalamu wawe macho ili maweye walindwe

–     Kizazi cha sasa wasiige wenye kutaka kugandamiza Kiswahili

–     Barakala wapigwe vikali

–     Ifanywe lugha murwa/ rasmi bungeni

–     Sindano kipigwe kikipatwa na maradhi                                                                                 

  • Anazungumza na kizazi cha kisasa ili waitunze, kuitukuza na kulinda Kiswahili

Anazungumza juu ya kule kuhifadhi lugha ya Kiswahili                                                      

  • Takriri- Kibwagizo kinarudiwarudiwa kutilia mkazo

Tashihishi-mfano: “kipatwa na maradhi kipigwe sindano” (lugha-uhai)

Chuku-Uzuri wa lugha umeongezwa chumvi                                                                        

  • Muenge-Kujitayarisha/ kujihadhirisha

Barakala-Wanaoiga desturi ya kigeni

Mfawadhi-Jitihada

Maamuma-Watu waja                                                                                                           

9.         a)         Kwa vyovyote vile kile anachoona ni chake na ni halali kwake ataitetea mpaka apate/ apewe

  • SAKARANI   – Sababu beti la Takhmisa na la Tarbia zimechanganywa kuitunga

-Ubeti wa kwanza ni wa aina ya takhmisa (mishororo mitano) na ubeti wa pili ni Tarbia

-Ubeti wa pili una mishororo minne na vina vya ndani ni tofauti

                        Mizani ni nane ukwapi na utao (16 kwenye mshororo)

                        Uhuru wa lugha k.m taidai badala- nitadai                                                                

  • Yu tayari kufanya kila jambo hata ikiwa ni kwa ncha ya upanga ikiwa mlimani, baharini, yu tayari kufuatilia                                                                                                          
  • Msanii anawapa motisha wasanii wake wawe wakiishi wakijua haki zao ni lazima wapewe la sivyo waitetee kwa vyovyote vile                                                                              
  • Mwandishi anasema kuwa izingirwe na ilindwe vilivyo kwa udi na ambari na mabawa lazima haki itunzwe ili isipokonywe au isiponyoke kwani mwanaume inajulikana akiwa hivyo
  • Mata- Kifo

Maizi- Cha manufaa/ dhamana

Fususi-Mchungaji   

Ushairi KCSE Questions And Answers                                                                                                                

USHAIRI WA 7

6.         i)          Una moyo gani                        N’nakuuliza                 Wangu mhisani

                        Na kiasi gani                           Unavyojiweza             Ijapo tufani

                        Ukiwa laini                              Utajipoteza                  Usijibani

                                    Kusimama   Pweke   Kwataka     Makini

            ii)         Zitavuma pepo                        Zitapupuliza                Uanguke chini

                        Ela uwe papo                          Unajikweleza              Na kujiamini

                        Utikiishapo                              Umejiuiza                    Pigo la moyoni

                                    Kusimama    Pweke    Kwataka    Makini

            iii)        Utie migati                              Ya kutuoteza               Hapo aridhini

                        Kwa nia na dhati                     Usiogeuza                   Au kuihini

                        Zidate baruti                            Uwe wapuuza             Welele usoni

                                    Kusimama   Pweke     Kwataka     Makini

            iv)        Sishike vishindo                      Na mauzauza               Ya kukuzaini

                        Kita kama nyundo                  Ukinuiliza                    Unayoamini

                        Na uje mkondo                       Utadikimiza                Kujipa mizani

                                    Kusimama   Pweke     Kwataka      Makini

            v)         Wengine wasiwe                     Unaoweleza                Yaliyo maani

                        Wewe ndiwe                           Unaoweleza                Yaliyo maani

                        Ela kichukuwe                        Pia kujikaza                 Katika midani

                                    Kusimama    Pweke     Kwataka       Makini

a)         Lipe kichwa shairi hili                                                                                                (al 2)

            b)         Kwa nini kusimama pweke “kwataka makini ’’                                              (al 2)

            c)         Ni hatua gani zinazopendekezwa mtu anayenuia kusimama pweke?                        (al 5)

            d)         Andika arudhi za shairi hili                                                                             (al 5)

            e)         Eleza msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa katika shairi hili                       (al 6)

  1. Muhisani
  2. Migati
  3. Vishindo
  4. Kweleza
  5. Mizani

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA USHAIRI WA 7

6.         a)         – Upweke wataka umakini                                                                             

                        – Upweke ni uvundo                                                                                       (al 2)

b)         – Kwasababu matatizo au shida zinapomsonga mtu, asipokuwa na utulivu wa fikira basi   – “Yeye huvunjika moyo” kwa vile hapana mtu wa kushirikiana naye   (al 2)

c)         –           Mtu anastahili kuwa mwenye moyo mgumu/ wa ujasiri                   

            –           Awe tayari kusimama kwa udhabiti pindi shida zinapomkabili

            –           Ajiamini kwa lolote atendalo kwa imara

–           Awe si mtu wa kutenda mambo ovyo ovyo ambayo yanaweza kumshawishi akaingia mtegoni

            –           Awe mstahimilivu na mwenye msimamo dhabiti

            –           Awe tayari kudinda na siri za ndani

d)         i)          Lina beti tano                                                                         

            ii)         Kila ubeti una mishororo minne, minne

            iii)        Ukawafi- Lina vipande vitatu- ukwapi, utao na mwandamizi

            iv)        Kila kipande kina mizani 6, jumla 18 kila mshororo

            v)         Kibwagizo chenye kimefupishwa mizani 12

            vi)        Vina vya ukwapi vinabadilika badilika. Vina vya utao na mwandamizi  

                        vinatiririka

e)         Mhisani – Mtu mwema                                                                                  

            Migati – Vizuizi

            Mkindo – Mw

            Unajikweleza –

USHAIRI WA 8

Soma shairi lifuatalo na kisha ujibu maswali yafuatayo.

UKUBWA JAA

Dunia yetu dunia, watu wanakufitini,                                                                                     Dunia huna udhia, watu wanakulaani,                                                                         Dunia huna hatia, wabebeshwa kila zani,                                                                               Dunia unaonewa, umetenda kosa gani!

Dunia umenyamaza, umetua kwa makini,                                                                    Dunia vitu mejaza, watu wanataka nini?                                                              Dunia wanakucheza,binadamu maluuni,                                                                                  Dunia unaonewa, umetenda kosa gani!

Dunia mtu akose, hukutia mdomoni,                                                                                       Dunia hebu waase, hao watu mafatani,                                                                                    Dunia chuki mpuse, muipate afueni,                                                                            Dunia unaonewa, umetenda kosa gani!

Dunia una lawama, za uongo si yakini,                                                                        Dunia wanokusema, ni manjunju si razini,                                                                             Dunia huna hasama, waja ndio kisirani,                                                                  Dunia unaonewa, umetenda kosa gani!

Dunia kuharibika, hayo amezusha nani?                                                                      Dunia watu humaka, hao wanokuhini,                                                                                               Dunia umejazika, kila tunu ya thamani,                                                                     Dunia unaonewa, umetenda kosa gani!

Dunia unatukisha, bwerere bila undani,                                                                                   Dunia unatukosha, maji tele baharini,                                                                          Dunia unaotehsa, mimea tosha shambani,                                                                  Dunia unaonewa, umetenda kosa gani!

Dunia hujageuka, tangu umbwe na manani                                                                  Dunia watu ndo, nyoka, mahaini na wahuni                                                               Dunia una baraka, mwenye pupa hazioni                                                              Dunia huna ubaya, wabaya ni insani.

Maswali:

(a) Shairi hili ni la bahari gani? Toa sababu yako.                                                   (alama 3)

(b) (i) Kichwa cha shairi hili kinaoanaje na maudhui ya shairi?.                              (alama 2)

(ii) Andika methali moja inayoeleza maudhui ya shairi hili.                                      (alama 3)

      (c)Eleza sifa tatu za wanadamu kama anavyoeleza mshairi.                                   (alama 3)

(d)Kwa kutoa mifano kutokana na shairi hili, eleza mbinu tatu za lugha alizotumia
mshairi.                                                                                                           (alama 6)

(e) Eleza maana ya vifungu vifuatavyo vya maneno kama vilivyotumika katika shairi.
(i) bwerere bila undani
(ii) hao watu mafatani
(iii) afueni
(iv) insani                                                                                                       (alama 4)

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA USHAIRI WA 8

1.

(a) Ni bahari ya kikwamba neno dunia limerudiwa mwanzoni mwa kila mshororo. Bahari nyingine ni ukara, kwa kuzingatia mwanzo, mloto, na mleo, vina vya ukwapi vinabadilika bali cha utao hakibadiliki. Pia, kuna manthawi, mistari ina ukwapi na utao (vipande viwili).                                                                   

 (b)            (i)        Kutokana na ukubwa wake, dunia inatupiwa lawama kwa maovu, udhia na hatia za kila

                        aina. Dunia inalinganishwa na jalala la kutupia taka.

 (ii)       Mbaazi ukikosa kuzaa husingizia jua.

  (c)           Binadamu hawapendi kulaumiwa.

Wana kisirani

Ni wahuni, wahaini

Ni waongo.

 (d)            Mbinu za lugha:-

Takiri – neno dunia limerudiwarudiwa na pia kibwagizo.

Dunia umeonewa, umetenda kosa gani?’

Tashhisi – Dunia imehuishwa kama mfano:- “Dunia hebu waase inaombwa itoe

mawaidha kwa walimwengu. Isitiara – ‘Dunia watu ndo nyoka’.

Watu wanalinganishwa na nyoka

 (e)       Maana ya vifungu:

Bwerere – bila undani – bure pasipo chuki, kinyongo.

Hao watu mafatani – hao watu wafitini

Afueni – nafuu, afadhali

Insani – watu, binadamu.

USHAIRI WA 9

1.          Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Jama, Jama, Jamani

            Mbona twabebeshwa mateso hivi

            Mizigo mikubwa ya dhiki kama

Kwamba hatuna haki ya kusema

Kukataa ndoa za lazima

Kukataa kuozwa wazee

Kukataa kukatishwa masomo

Kukataa tohara ya lazima

Jama, Jama Jamani

Iweje tuteswe mateso haya

Na watu wasio kuwa hata na haya kama

Kwamba hatuna haki ya kulalamika

Kulalamikia kutumikishwa kama mayaya

Kulalamikia kudhalilishwa kiunyama

Kulalamikia kutolindwa na sheria

Jama, Jama, Jamani

Sasa hii ni awamu nyingine

Na macho tumeyafungua kabisa

Tumekataa kudhalilishwa kabisa

Tumekataa kuteswa kama watumwa

Tumekataa tohara ya lazima

Tumekataa kuozwa……. Tumekataa! Tumekataa

Hii awamu ya ’Haki ya mtoto wa kike’

Maswali

a) Taja mambo matatu muhimu yaliyozungumzwa na mshairi kisha ueleze kila

    moja.                                                                                                           (Alama 6)

b)         Eleza muundo wa shairi hili                                                                (Alama 4)

c)         Taja mbinu mbili za lugha alizotumia mshairi kisha ueleze kila moja(Alama 4)

d)         Kwa nini mshairi huyu anasema hii ni ’awamu’ nyingine?               (Alama 3)

e)         Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa na mshairi  (alama 3)

  • awamu
  • kudhalilishwa
  • Dhiki

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA USHAIRI WA 9

  1. a) SHAIRI

Mambo matatu muhimu yaliyozungumziwa na mshairi na maelezo ya kila moja.

Kutaja alama 1

Kueleza alama 1

Jumla ( alama 6)

i) Mateso

-Mizigo mikubwa ya dhiki

-Hakuna haki ya kunena

ii) Ndoa ya lazima

-Kuozwa kwa wazee

-Kukatishiwa masomo

iii) Tohara

-Tohara ya lazima

-Hawaruhusiwi kusema chochote

iv) Sheria

-Haiwalindi

-Kudhalilishwa kinyama

v) Awamu tofauti

-Wamekataa kudharauliwa

-Wamekataa kuteswa

-Wamekataa  tohara za lazima.                                                                      

  • Muundo wa shairi

i)Ni wimbo ambao haufuati muundo wowote wa ushairi

ii)Ni shairi huru

iii)Halina mpangilio wowote wa kiarudhi

iv)Halina mgao wa mishororo

v)Halina vina wala mizani

vi)Halina kibwagizo

vii) Lina beti 3

viii)Mishororo si sawa  katoka kila ubeti                                                                  

     c.   Mbinu mbili za lugha alizotumia mshairi. Maelezo ya kila moja

            i) Nyimbo-Amezitumia Kwa njia mwafaka ili anase hisia za wasomaji.

            ii) Takriri-Amejaribu pia kusisitiza ili kuwekea uzito yale anayozungumzia.

-Anataka msomaji apate mvuto mzuri kwa lile analolizungumzia. Mfano tumekataa kudhalilishwa, tumekataa kuteswa, tumekataa tohara.

            iii) Mdokezo. Mfano Tumekataa kuozwa …

            iv) Tashbihi . mfano ubeti wa pili- Kutumikishwa kama yaya

       d.   Sababu za mshairi kusema; ‘hii ni awamu nyingine’

            i)Ulikuwa ukurasa mpya wa maisha.

            ii)Kuna mabadiliko ya kuondoa ukandamizaji.

            iii)Wanawake wamekataa kuozwa kwa lazima.

            iv)Wamekataa kudhalilishwa kabisa                                     

       e.  Maana ya maneno

i)) awamu-Kipindi

ii) kudhalilishwa-kukandamizwa/ kudunishwa / kufedheheshwa

  1. dhiki-shida     

USHAIRI WA 10

 Soma shairi lifuatalo  kisha ujibu maswali yafuatayo

  1. Mkata ni mkatika, harithi hatoridhiwa

Sina ninalolishika, wala ninalochukuwa

Mlimwengu kanipoka, hata tone la muruwa!

Mrithi nini wanangu?

  •  Sina ngo’mbe sina mbuzi, sina konde sina buwa

Sina hata makaazi, mupasayo kuyajuwa

Sina mazuri makuzi, jinsi nilivyoachwa

Mrithi nini wanangu?

  •  Sina kazi sina bazi, ila wingi wa shakawa

 Sina chembe ya majazi, mno nikukamuliwa

 Nakwa’cheni upagazi, ngumu kwenu ku’tuwa

Mrithi nini wanangu?

  •  Sina sikuachi jina, mkata hatasifiwa

Hata nifanye la mana, mno mi kulaumiwa

Poleni wangu sana, sana kwenu cha kutowa

            Mrithi nini wanangu?

  • Sina leo sina jana, sina kesho kutwaliwa

Sina zizi sina shina, wala tawi kuchipuwa

Sina wanangu mi sina , sana la kuacha kuraduwa

            Mrithi nini wanangu?

  •  Sina utu sina haki, mila yangu meuliwa

Nyuma yangu ili dhiki, na mbele imekaliwa

N’nawana na miliki, hadi nitakapofukiwa

            Mrithi nini wanangu?

  •  Sina ila kesho kwenu, wenyewe kuiongowa

Muwane kwa nyinyi mbinu, mwende pasi kupumuwa

Leo siyo kesho yenu, kama mutajikamuwa

Mrithi nini wananngu?

  • Taja mambo yoyote mawili ambayo mtunzi angewarithisha wanawe.                    (alama 2)
    •  Eleza sababu ya mtunzi kutoweza kuwarithisha wanawe.                                                   (alama 3)
    •  Andika ubeti wa nne kwa lugha nathari.                                                                 (alama 4)
    •  Dondoa mifano miwili miwili ya :                                                                           (alama 2)
      • Inkisari
      • Tabdila
    • Chambua shairi hili kwa upande wa :
      • Dhamira                                                                                                                   (alama 2)
      • Muundo                                                                                                                   (alama 4)
  • Eleza maana ya vifungu vifuatavyo kama vilivyotumiwa katika shairi.                (alama 3)
    • Mlimwengu kanipoka
      • Sina konde sina buwa.
      • Wingi wa shakawa.

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA USHAIRI WA 10

  • –    Makazi mabovu

–     Upagazi

–     Kutothaminiwa

–     Dhiki

–     Kufanya kesho ya wengine nzuri

  • –     Ni maskini hohehahe / hana kitu

–     Aliporwa kila kitu.

–     Hana  mifugo.

–     Hana kazi yoyote.

–     Hana sifa / umaarufu.

–     Ana makazi mabovu.

  • –     Sina jina nitakawacha kwani maskini hasifiwi

–     Hata nikifanya jambo la maana ninalaumiwa tu.

–     Poleni sana wanangu kwa kuwa sina la kuwatolea.

–     Mtarithi nini wanangu?

  • (i) Inkisari                        
  • Mana – Maana
  • Meuliwa – Imeuliwa
  • Nitapofukiwa – Nitakapofukiwa.

            (ii) Tabdila

                  Muruwa           – Murua

                  Kutowa           -Kutoa

                  Kuchipuwa      -Kuchipua

                  Kuiongowa     – Kuiongoa

                  Kupumuwa     – Kupumua

  • (i) Dhamira
  • Kuwahimiza watu kufanya bidii wakiwa vijana.
  • Kulalamika kwamba maskini hana haki / huonewa / hapewi nafasi. 

     (ii) Muundo

  • Shairi ni aina ya tarbia / unne.Lina mishororo minne katika kila ubeti.
  • Mishororo ya kwanza mitatu imegawika  katika sehemu mbili (ukwapi na utao).
  • Kila kipande kina mizani nane na kila mshororo una mizani kumi na sita.
  • Vina vya kati vinatofautiana kutoka ubeti mmoja hadi mwingine, lakini vina vya mwisho ni sawa katika shairi zima katika mishororo ya kwanza mitatu.
  • Shairi hili lina kibwagizo ambacho kimefupishwa.

Mrithi nini wanangu?

  •  Shairi hili lina beti saba.
  •  (a) Mlimwengu kunipoka – Mlimwengu kanipokonya.

(b) Sina konde sina buwa – Sina shamba sina chochote.

(c) Wingi wa shakawa – mashaka mengi.

Ushairi KCSE Questions And Answers-Questions 1-5

Scroll to Top