Please Limited time Offer!

KCSE Ushairi Revision Question

MASWALI

Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.  

Zitavuma, 

Zitakoma, 

Nitakwima,  Mti-mle. 

Na muda nikisimama, 

Nitatongoa nudhuma,  Kwa tenzi zilizo njema,  Nilisifu mti – mle. 

Tazipanga tathlitha, tungo zilizo na hekima,  Za huba na thiatha, za kuburudi mitima,  Mashairi mabuthutha, musome mnaosoma. 

Mti nishainukia,namea kuwa mzima, 

Mizizi yadidimia, ardhini imeuma,  Nanena kitarbia, tungo zilizo adhama  Japo ni tungo za zama, mti-mle hutumia. 

Zingavuma zitapusa, pepo kali zitakoma, 

Dharuba kinitikisa, mti-mle huinama, 

Huyumba nikaziasa, matawi yakakingama, 

Gharika ikishapisa, hurudi nikawa wima,  Na tungo za takhimisa, mti-mle huzipima. 

Maswali  

  • Shairi hili ni la kimapokeo. Toa sababu mbili kuunga kauli hii.             (Alama.2) 
  • Taja bahari kuu ya ushairi ambayo imetumiwa na mshairi. Fafanua(Alama.2)  (c) Fafanua dhamira ya mshairi.         (Alama.2) 
  • Kwa kutoa mifano bainisha tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi hili. 

(Alama.2) 

  • Eleza jinsi mshairi ametumia idhini ya ushairi katika utungo huu.   (Alama.2) 
  • Andika ubeti wa nne kwa lugha natharia.                                     (Alama.4) 
  • Mshairi anamaanisha nini anaposema ‗zingavuma zitapusa, pepo kali zitakoma,‘(Al2) 
  • Eleza toni ya shairi hili.                                                                (Alama.2) 
  • Eleza maana ya msamiati ufuatao. 
    • Nitatongoa 
    • Zitapusa.                                                                                         (Alama.2)

KCSE USHAIRI 2

MASWALI

USHAIRI.

             Soma shairi hili kisha ujibu maswali.

            Sinusubuwe akili, nakusihi e mwandani

            Afiya yangu dhahili, mno nataka amani

 Nawe umenikabili, nenende sipitalini  Sisi tokea azali, twende zetu mizimuni  Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani?

            Mababu hawakujali, wajihisipo tabani

            Tuna dawa za asili, hupati sipitalini

       Kwa nguvu ya kirijali, mkuyati uamini        Kaafuri pia kali, dawa ya ndwele fulani        Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani.

            Mtu akiwa halali, tumbo lina walakini

            Dawa yake ni subili, au zogo huauni

          Zabadi pia sahali, kwa maradhi yalo ndani Au kwenda wasaili, wenyewe walo pangani

Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani

            Mtu kwenda sipitali, nikutojuwa yakini.

            Daktari kona mwili, tanena kansa tumboni

          Visu vitiwe makali, tayari kwa pirisheni  Ukatwe kama figili, tumbo nyangwe na maini

Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani

Japo maradhi dhahili, kuteguliwa tegoni,

Yakifika sipitali, huwa hayana kifani

Waambiwa damu, kalili ndugu msaidieni

Watu wakitamali, kumbe ndio buriani

Nifwateni sipitali, na dawa ziko nyumbani

Mizimu wakupa kweli, wakueleze undani

Maradhiyo ni ajali, yataka vitu dhamani

Ulete kuku wawili, wamajano na wa kijani Matunda pia asali, vitu vyae chanoni Nifwateni sipitali, na dawa zi mlangoni?

MASWALI.

  1. Lipe shairi hii anwani mwafaka.                                                     (al.1)
  2. Toa sababu zinazofanya mshairi kutokana kwenda hospitali.                  (al.3)
  3. Andika ubeti wanne kwa lugha ya nathari/ tutumbi.                                (al.4)
  4. Taja bahari mbili zilizotumika katika shairi hili.                                (al.2)
  5. Tambua nafsineni katika shairi hili.                                                         (al.1)                 
  6. Tambua toni ya shairi hili.                                                                        (al.1)    
  7. Eleza muundo wa shairi hili.                                                               (al.4)
  8. Fafanua uhuru wa mshairi unavyojitokeza katika shairi hili.            (al.2)
  9. Andika maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi hili. 

                                                                                                                            (al.2)

(i)Dhalili

                         (ii) Azali

KCSE USHAIRI 3

MASWALI

       Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.   (alama 20)  Barabara.

            Barabara bado ni ndefu

            Nami tayari nimechoka tiki

            Natamani kuketi

            Ninyooshe misuli

             Nitulize akili

            Lakini

            Azma yanisukuma

            Mbele ikinihimiza kuendelea

       Baada ya miinuko na kuruba        Sasa naona unyoofu wake        Unyoofu ambao unatisha zaidi.

            Punde natumbukia katika shimo 

            Nahitaji siha zaidi ili kupanda tena,

       Ghafla nakumbuka ilivyosema  Ile sauti zamani kidogo

            “Kuwa tayari kupanda na kushuka”.

            Ingawa nimechoka 

            Jambo moja li dhahiri

            Lazima niifuate barabara

            Ingawa machweo yaingia

            Nizame na kuibuka

            Nipande na kushuka

       Jambo moja nakumbuka: Mungu        Je, nimwombe tena?  Hadi lini?  Labda amechoshwa na ombaomba zangu         Nashangaa tena!

            Kitu kimoja nakiamini

            Lazima niendeleee kujitahidi kw akila hatua mpya

            Nijikokote kuiandama hii barabara yenye ukungu

            Nikinaswa na kujinasua,

            Yumkini nitafika mwisho wake

            Ikiwa wangu mwisho haitauwahi kabla.

                                           (Timothy Arege)

Maswali:

  • Taja na ueleze aina ya shairi hili.                                                       (alama 2)
  • Eleza toni ya shairi hili.                                                            (alama 2)
  • Fafanua dhamira ya shairi hili.                                                 (alama 2)
  • Bainisha vipengele vifuatavyo vya kimtindo katika shairi hili.                    (alama 3)
    • Tanakali za sauti
    • mbinu rejeshi
    • Taswira
  • Eleza umuhimu wa maswali balagha katika shairi.                  (alama 2)
  • Andika ubeti wa mwisho kwa lugha nathari.                            (alama 4)
  • Eleza matumizi ya mistari mishata katika shairi hili.                          (alama 2)
  • Eleza maana ya misamiati ifuatayo kama ilivyotumika katika shairi. (alama 3)
  • Kuruba
    • siha
    • machweo

KCSE USHAIRI 4

MASWALI

Soma shairi hili kisha ujibu maswali

  1. Punda kalibebe gari, gari limebeba punda Mwalimu ana pakari, muashi vyuma adunda Jaji gonga msumari, sonara osha vidonda.

Kinyume mbele

  • Saramala ahubiri, muhunzi tiba apenda

Mganga anaabiri, baharini anakwenda

Hata fundi wa magari, anatomea vibanda

Kinyume mbele

  • Wakili anahiyari, biashara kuitenda Mtazame askari, akazakaza kitanda,

Mkulima mashuhuri, jembe limemshinda

Kinyume mbele

  • Apakasa daktari, ukili anaupinda

Saveya kawa jabari, mawe anafundafunda,

Hazini wa utajiri, mali yote aiponda,

Kinyume mbele

  • Msemi huwa hasemi, wa inda hafanyi inda

Fahali hawasimami, wanene waliishakonda

Walojitia utemi, maisha yamewavunda

Kinyume mbele

  • Kiwapi cha kukadiri, twavuna shinda kwa shinda

Tele haitakadari, huvia tulivyopanda

Mipango imehajiri, la kunyooka hupinda Kinyume mbele 

MASWALI
  1. Mtunzi alikuwa na malengo gani alipotunga shairi hili?                          (alama 3)
  2. Licha ya tarbia, eleza bahari nyingine zinazojitokeza katika shairi hili. (alama 4)
  3. Eleza namna mtunzi alivyoutumia uhuru wake.                                        (alama 5)
  4. Ni mbinu gani inayotawala shairi hili?                                                    (alama 2)
  5. Uandike ubeti wa nne katika lugha nathari.                                             (alama 4)
  6. Eleza toni ya shairi hili.                                                                            (alama 2)

KCSE USHAIRI 5

MASWALI

Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali

Ulimwengu ulimwengu, ulimwengu naratibu

Yaliyo kichwani mwangu, nataka kuyatubu Wayasome ndu zangu, wa mbali na wa karibu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Ulimwengu ni kiwanja, cha wenye raha na tabu

Wengine wanajikonja, kwa wengine ni adhabu Kucha na kutwa twahanja, kutafuta matulubu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Ni uwanja wa balaa, aliniusia babu

Mna mambo yamejaa, ya faraja na kusibu Na machache ya kufaa, ila mengi ya udubu Cha wenye raha na tabu,ulimwengu ni kiwanja.

Ni kiwanja cha Amina,Saidi Ali Rajabu

Wengine kitu hatuna, tunaishia kababu Wale wamejaza sana, wanashindwa kuhesabu Cha wenye raha na tabu, Ulimwengu ni kiwanja.

Ni uwanja wa urongo, na kweli pia ajabu

Kichwa hudanganya shingo, tumbo kiuno chasibu Usitumai ubongo, wa nduguyo na swahibu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Ni uwanja wa walevi, pombe kwao ni dhahabu

Mara vile mara hivi, wakilewa majudhubu Maneno ya kiujuvi, hujipaka hata shabu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Ni  kiwanja wenye dini, wamtiio wahabu

Mashekhe msikitini, humo humfanya muhibu

Mapadiri kanisani, huvihubiri vitabu

Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Ni uwanja wa malofa, lofa mtu mwenye tabu

Kusema sana kashifa na moyo kisebusebu Tunakaribia kuja, kwa kushindwa kujimudu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Ni uwanja wa faraja, alowajali habibu

Na wengine sitotaja, msinambe ninagubu Ni uwanja wa viroja, vigumu kuvikutubu

Cha  wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.

Maswali

(a)Lipe shairi hili anwani ifaayo.                                                                        (alama 1)

 (b) kwa kutoa mfano, eleza mbinu zozote mbili za lugha zilizotumika katika shairi.

                                                                                                       (alama 2)

(c)Eleza jinsi uhuru wa mshairi ulivyotumika katika shairi.                               (alama 2)

 (d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi.                                                    (alama 4)

 (e)Taja na ueleze bahari zozote mbili zilizotumika katika shairi hili.                (alama 2)

 (f)Eleza umbo la shairi hili.                                                                     (alama  4)

 (g)Eleza toni ya shairi hili.                                                                      (alama 1)

 (h)Fafanua dhamira ya mshairi.                                                                  (alama 2)  (i)Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi.        (alama 2) (i) Malofa:

 (ii) Udubu:

Scroll to Top