Please Limited time Offer!

Mbinu za Uandishi katika Mapambazuko

Mbinu za Uandishi (Mwongozo wa Mapambazuko ya Machweo)

Tashbihi

Atakuja tu, labda ghamidha itakuwa imezidi, imefura kama hamuri lililotiwa hamira. Sasa kucheka kwake kulikuwa nadra kama kupatwa kwa mwezi.

Swali likajitunga akilini mwake, na kama mwangwi, likawa linajirudia tena na tena. Shati lenyewe limekuwa mararu, limemganda kama kigaga.

Watoto waliokuwa na hamu kutoka nje wakawa watulivu kana kwamba viti vimekuwa sumaku. Wamefika nusu safari, bintiye katulia kama maji mtungini.

Sasa kazi kukilea kitoto chao, kibinti hiki kilichomlanda mamake kama shilingi kwa ya pili. Badala yake liliuchochea, kama moto kuvuvia.

Nia yangu nyeupe kama pamba.

Sasa mumewe anataka kujisiriba uchafu ule na kama mchezea tope, atarukiwa tu. Ona umbo lako sasa, kama nguruwe.

Kisha kofi likaandamwa na teke lililomlaza kochini kama zigo lililosukumwa likajiangukia ovyo. Ilikuwa kama kuchokoza nyuki.

Lilia alimfungulia mlango akitetemeka kama unyasi upepo uvumapo.

Tashihisi- Mbinu Katika Mapambazuko ya Machweo

Saa ukutani ilimwambia saa nane za usiku,

Fikra zimechoka, mwenyewe hajiwezi; nusura yake usingizi uliomsomba, ukampa utulivu, japo wa muda tu.

Kama si ulimi wa bintiye ambaye hatulii, kihoro kingemvamia labda hata kumvuta kuelekea kaburini. Lakini hawakujua ajali ya barabara ingeyafuta maisha ya mama mtu. Nguo zilezile, usafi bado unampiga chenga. Lakini dhiki ziliwaandama.

Istiara

Isije ikawa mwenye nyumba kaja na yeye mpangaji akachelewa kumfungulia mlango. Mbona Luka akageuka kuwa mzigo wa moto, habebeki, habebeki kamwe?

Yamekolezwa ladha na sauti, asali kando.

Akatamani kufika nyumbani apumzike, kazi ya kuwalisha kondoo wa Mungu si kazi rahisi.

Lilia, malaika wake, hampi utulivu wa kuwazia sana kuhusu upweke wake. Naye wembe masomoni, akili zake sumaku, hunasa yote wafunzayo walimu. Kaloa, katota hili penzi la jogoo la mji.

Na ule ulimi wake uliodondoka asali, waumini wakampenda. Kwake siasa ni mchezo mchafu.

Lilia akatambua rangi halisi ya mumewe. Tamaa ndiyo ibada yake, Ulaghai sasa ndiyo ibada yake kubwa, mhubiri keshakuwa mhadaifu.

Ulimfanya mkeo ngoma kwa sababu ya hawara ambaye hakuthamini hata chembe.

Semi na Nahau Katika Hadithi: Mapambazuko

roho mkononi, pumzi zikimwenda mbio- yaani kwa wasiwasi tele. nyanyaso moto mmoja- yaani

tele, zisizokoma.

hakuwa na budi- alilazimika, hakuwa na lingine yalikuwa yale yanayodaiwa kumtoa nyoka pangoni- yalivutia sana akawa hoi- akachoka sana.

kufunga pingu za maisha- kuoana. unampiga chenga- unamhepa rafiki yake wa kufa kuzikana- rafiki mkubwa/wa dhati.

binti hasikii la mwadhini wala la mteka maji msikitini- hasikii lolote wala yeyote. kumvunja

moyo- kumuumiza hisia. wakafunga pingu za maisha- wakaoana. Lilia alipigwa na butwaa- alishangaa alipokataa katakata-

alipokataa kabisa. kumuunga mkono- kumsaidia kutimiza azma yake, kukubaliana naye. hajali habali- hajali hata kidogo, hajali chochote. utajua kilichomtoa kanga manyoya shingoni- utaingia mashakani/utaumia. Akamkaribisha kwa

mikono miwili- akamkaribisha vizuri, kwa ukuruba mzuri. amepata nafuu- hali yake imeimarika/ afya yake imeimarika aage dunia- afariki, akufe.

Scroll to Top