JIBU MASWALI YOTE
- Haki za watoto zina maana au umuhimu gani? (alama 2)
 - Zinawezesha watoto wote katika himaya zao kunufaika
 - Taja haki tano ambaza mtoto anatakiwa kuwa nazo kulingana na kifungu. (alama5)
 - Kuishi na kupata chakula chenye lishe bora
 - Kupata elimu
 - Kutopigwa na kutumikishwa
 - Kutalazimishwa kufanya kazi
 - Kuishi katika nyumba na makazi bora
 - Eleza mifano mitatu kuonyesha jinsi haki za watoto zinavyokiukwa. (alama 3 )
 - Kutekwa na kutumikishwa vitani
 - Kufanyishwa kazi kipunda
 - Kupigwa na kinyimwa chakula
 - Kuishi katika mazingira hatari
 - Unadhani ukiukaji wa haki za watoto unaweza kuepukwaje? (alama 2)
 - Serikali kushirikiana na kuhakikisha watoto wote wamo shuleni kwa kuhakikisha elimu ya bure.
 - Kupeleka miswada bungeni kuhusu haki za watoto na kupitisha kwa bsheria.
 - Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika: (alama 3)
 - Mkataba
 - Makubaliano kuhusu kitu/jambo Fulani
 - Ukiukaji
 - Kutenda kinyume na sharia/ makubaliano Fulani.
 - Lindi la ufukara
 - Umaskini
 
SEHEMU YA B: SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA
- Taja aina mbili za sauti za Kiswahili. (alama 2)
 - Konsonanti
 - Irabu
 - Onyesha shadda katika maneno yafuatayo. (alama 2)
 - Cherehani
 - Chere’hani
 - Kitabu
 - Ki’tabu
 - Ainisha viambishi katika neno lifuatalo. (alama 3)
 
Tutakayempelekea
Tu ta ka ye m pelek e a
Kiambishi kiambishi kiambishi kirejeleo mtendwa mzizi mnyambuliko kiishio
cha nafsi cha wakati cha wakati
- Kanusha sentensi zifuatazo. (alama 2)
 - Ningesoma ningepita.
 - Nisingesoma nisingepita
 - Ningalikuwa na uwezo ningalimsaidia.
 - Nisingalikuwa na uwezo nisingalimsaidia.
 - Andika sentensi ifuatayo kwa udogo kisha katika wingi. (alama 2)
 
Mtoto mkaidi aliiba kitabu cha mwenzake.
- udogo – Kitoto kikaidi kiliiba kijitabu cha mwenzake.
 - wingi – Vitoto vikaidi viliiba vijitabu vya wenzao.
 - Onyesha viwakilishi katika sentensi zifuatazo, (alama 2)
 - Yule na huyo wamemaliza kazi yao.
 - Chenyewe kimekaliwa na wageni wake.
 - Akifisha sentensi ifuatayo. (alama 3)
 
mama maria amenunua kabeji kitunguu mchicha sukumawiki na sufuria.
- Mama Maria amenunu; kabeji, kitunguu, mchicha, sukumawiki na sufuria.
 - Andika sentensi zifuatazo katika wakati ujao. (alama 2)
 - Mama ameninunulia kalamu.
 - Mama ataninunulia kalamu.
 - Wanafunzi wameenda nyumbani.
 - Wanafunzi wataenda nyumbani.
 - Nomino hizi zipo katika ngeli gani? (alama 2)
 - Mwezi
 - U – I
 - Maji
 - YA – YA
 - Andika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa. (alama 2)
 
“Uhuru huu tunaojivunia ulipatikana kwa umwagikaji mwingi wa damu,” mwanasiasa alisema.
- Mwanasiasa alisema kuwa uhuru huo waliojivunia ulipatikana kwa umwagikaji mwingi wa damu.
 - Unda nomino kutokana na vitenzi vilivyo mabanoni ili kukamilisha sentensi zifuatazo. (alama 2)
 - ………………Ndoto………………………ilikuwa ya kuogofya mno. (ota)
 - Jengo hili lilijengwa na ………mjenzi/mjengo/ujenzi…………………………………..hodari. (jenga)
 - Tunga sentensi sahihi ili kutofautisha maana ya vitate vifuatavyo. (alama 2)
 
Suka – kutengeneza ukili au nywele
Zuka – kutokea kwa kitu/ jambo ambalo halikuwepo.
- (Mwalimu ahakiki majibu ya mwanafunzi ambapo atatunga sentensi)
 - Tumia kivumishi ‘-enyewe’ kukamilisha sentensi zifuatazo. (alama 2)
 - Mimi nataka mikate yenyewe
 - Manukato ………yenyewe…………………………yananukia.
 - Bainisha maneno katika sentensi ifuatayo. (alama3 )
 
Yusufu na Ali wamekwenda wapi jamani?
- Neno ‘huyu’ limetumikaje katika sentensi hizi? (alama 2)
 - Huyu amekuja kwangu.
 - kiwakilishi
 - Mgeni huyu amekuja kwangu.
 - kivumishi
 - Onyesha vivumishi katika sentensi zifuatazo. (alama 4)
 - Tunda kubwa limeanngukia mtoto mvivu.
 - Shule maarufu husajili wanafunzi wengi.
 - Taja aina tatu za nomino huku ukizitolea mifano. (alama 3)
 - Nomino za pekee
 - Nomino za dhahania
 - Nomino za kawaida
 
(Mwalimu ahakiki mifano)
18. Andika kwa wingi.
Upepo wa kusini ulipeperusha mabati ya paa la nyumba na kuharibu kifaamuhimu. (alama 2)
- Upepo wa kusini ulipeperusha mabati ya paa za nyumba na kuharibu vifaa muhimu.
 
19. Tofautisha kati ya shadda na kiimbo. (alama 2)
- Kiimbo ni kupanda na kushuka kwa sauti wakati mtu anapoongea – kiimbo
 
20. Tunga sentensi yenye mpangilio ufuatao. (alama 2)
Nomino + Kivumishi + Kitenzi + Kielezi + Kielezi
- Mwanafunzi mtukutu aliadhibiwa vikali sana.
 
21. Taja na ueleze aina mbili za ala za matamshi (alama 4)
Toa mifano kwa kila aina.
- Ala sogezi – viungo vinavyosonga wakati wa kutamka : mfano, ulimi na midomo
 - Ala tuli – viungo ambavyo havisogeisogei wakati wa kutamka: mfano, meno na ufizi.
 
SEHEMU YA C: FASIHI SIMULIZI
- (a) Taja aina zozote tano za nyimbo. (alama 5)
 - Nyimboza kazi
 - Nyimbo za watoto (bembelezi)
 - Vifo
 - Nyiso
 - Kisiasa
 - Mbolezi
 
(b) Tofautisha kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi (alama 10)
Tofauti kati ya Fasihi Andishi na Fasihi Simulizi
| FASIHI SIMULIZI | FASIHI ANDISHI | |
| 1. | Huwasilishwa kwa njia ya mdomo na/au matendo. | Huwasilishwa kwa njia ya maandishi | 
| 2. | Ni mali ya jamii. | Kazi andishi ni mali ya mwandishi (na mchapishaji) | 
| 3. | Msimulizi anaweza kubadilisha sehemu Fulani | Kitabu kilichoandikwa hakiwezi kubadilishwa | 
| 4. | Huhifadhiwa akilini | Huhifadhiwa vitabuni | 
| 5. | Kazi simulizi hubadilika na wakati | Kazi andishi haibadiliki na wakati | 
| 6. | Huhitaji msimulizi na hadhira yake wawe mahali pamoja wakati wa masimulizi | Msomaji anaweza kusoma kitabu cha hadithi peke yake, mahali popote, wakati wowote | 
| 7. | Mtu yeyote anaweza kutunga na kusimulia | Ni lazima mwandishi na msomaji wawe na uwezo wa kusoma | 
| 8. | Hutumia wahusika wa aina zote. (wanyama, watu, mazimwi n.k) | Hutumia wahusika wanadamu. | 
| 9 | Ina tanzu na vipera vingi. | Tanzu na vipera ni chache ukilinganisha na Fasihi simulizi | 
| 10 | Ni kongwe. Imekuwa tangu mwandamu aanze kuishi duniani | Ilianza baada ya uvumbuzi wa maandishi. | 
| 11 | Huwasilishiwa mahali maalum km. Miviga kv arusi maabadini, tohara mtoni, kafara pangoni nk, | Kazi ya fasihi andishi yaweza kuwasilishwa au kuendelezwa popote. Msomaji wa riwaya anaweza kusomea apendapo. |